Breaking News

HALIMASHAURI YA WILAYA YA SINGIDA IMELENGA KUTOA ELIMU KWA WAKULIMA

 


Na. Wellu Mtaki, Dodoma 


Afisa ugani kilimo Halmashauri ya wilaya ya Singida Emanuel Ambrose amesema ushiriki wao kwenye maonesho ya wakulima (nane nane) yamelenga kutoa Elimu Kwa wakulima ili kuongeza tija kwenye uzalishaji.

Amesema kuwa kwenye vipando vyao wamehusika  mazao ya Alizeti,vitunguu pamoja na Mtama ambayo ni Mazao ya kibiashara Mkoani Singida.

 ambrose ameyasema hayo  Agosti 1, 2025 wakati anazungumza na Nico Media   Jijini Dodoma Katika  maonesho  nane nane .

Aidha   amefafanua  kuwa ukuaji wa Mazao hayo ya kitunguu, Alizeti pamoja na Mtama ambao kwa upande wa Alizeti pamoja na vitunguu huchukua siku 90 mpaka kuwa tayari kwa mavuno wakati Mtama ukichukua miezi 6.


Hata hivyo Afisa huyo amewaasa Wananchi wanaotembelea maonesho hayo ya nane nane wafike katika mabanda yao ya kilimo ili waweze kujifunza mbinu mbalimbali za kilimo kwa ajili ya kuongeza thamani ya kilimo chao.