Breaking News

TAARIFA ZA MAANDAMANO YA VIJANA WA KIZAZI KIPYA GEN -Z NCHINI NEPAL


Waziri Mkuu wa Nepal, KP Sharma Oli, amejiuzulu kufuatia hasira kali ya umma baada ya vifo vya watu 22 waliouawa kwenye makabiliano kati ya polisi na waandamanaji waliokuwa wakipinga ufisadi.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi yake, kujiuzulu kwake kumelenga kufungua njia ya kupatikana kwa suluhisho la kikatiba kufuatia maandamano makubwa yanayoongozwa na vijana, yaliyosababishwa na tuhuma za ufisadi uliokithiri na marufuku ya mitandao ya kijamii ambayo sasa yameondolewa.

Maandamano hayo yaligeuka kuwa ya vurugu siku ya Jumatatu, baada ya maelfu ya waandamanaji wengi wao wakiwa wamebeba mabango yaliyokuwa na maandishi kuwa ni vijana wa kizazi cha Gen Z, Waliingia barabarani jijini Kathmandu.

Inakadiriwa kuwa watu takriban 200 walijeruhiwa katika makabiliano hayo, ambapo polisi walitumia gesi ya kutoa machozi, magari ya maji ya kuwatawanya waandamanaji, na hata risasi za moto.