Breaking News

WANANCHI WAENDELEA KUTEMBELEA BANDA LA OFISI YA WAZIRI MKUU KATIKA VIWANJA VYA SABASABA






NA.MWANDISHI WETU - DAR ES SALAAM.

Wananchi mbalimbali wameendelea kutembelea  katika banda la Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Taasisi zake ili kupata elimu kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Ofisi hiyo katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama SABASABA yanayoendelea Jijini Dar es Salaam.

Aidha, wameonesha kuridhishwa na huduma zinazitolewa na ofisi hiyo pamoja na mambo mengine wamepata  elimu kuhusu masuala ya vijana, ajira ulemavu na Uratibu wa Shughuli za Serikali.

 Maonesho hayo kwa mwaka huu yana  Kauli Mbiu  inayosema “Maonesho ya Biashara ya Kimataifa sabasaba, Fahari ya Tanzania” leo tarehe 03 Julai, 2025.

MATUKIO KATIKA PICHA



(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)