Breaking News

PURA WAPAMBANA KUTOA AJIRA KWA VIJANA

 


Na Mwandishi wetu Saba Saba

TPDC imeshiriki kwa  40% ambapo 60% zimebaki kwa watu wa nje" alisema mhandisi

Mkurugenzi mkuu wa  mamlaka ya mkondo wa juu wa petroli Mhandisi wa petroli Charles Sangweni amesema amepongeza maonyesho ya 49 ya kimataifa ya biashara  ( Sabasaba) kwa sababu yamekuwa ya kisasa zaidi ( kidigitali ) ukilinganisha na vipindi vya nyuma.

Aidha mhandisi Sangweni aliongeze kwamba ameona mwamko wa wananchi umekuwa mkubwa katika banda la PURA  na mswali ambayo yanayoulizwa katika banda lao yamekuwa ya kisomi zaidi  ambayo maswali hayo yanaonesha wananchi wamekuwa na mwamko mkubwa kuhusiana na mafuta na gesi.


Awali kwa leo pia  alitembelea  banda la PURA na mabanda mengine aliona  mwamko  mkubwa wa wananchi upo kwenye nishati safi ya kupikia hivyo inaonesha wananchi wamepata elimu ya kutosha kuhusiana na umuhimu wa kutumia nishati safi.

"Tunafahamu kuwa hii agenda ya matumizi ya nishati safi ya kupikia  kinara wake ni mkuu wetu wa nchi  Dkt.Samia Suluhu Hassan na hata Kupitia kwa hiyo inanipa faraja sisi  watendaji wake tunafanya kazi kwa vitendo na hatumuangushi" alisema Sangweni 

Aliongezea  kwamba kazi kubwa ya  PURA ni  kukusanya data kwa ajiri ya kuangalia upatikanaji wa mafuta,

Kampeni ya kwanza ilifanyika katika maeneo ya bahari kuu 2018 ambapo tulichimba kisima kimoja, na kampeni kubwa ilikuwa katika maeneo ya uchimbaji kati ya wafanyakazi  150 tulikuwa na wafanyakazi 52 kwa mara ya kwanza kutoka ndani ya nchi na wengi walikuwa wamepata uzoefu kutoka nchi mbalimbali na projeti za ndani ya nchi.

" Sasa hivi tunakampeni inayoendelea endapo ipo kwenye maandalizi inaendelea ambapo  tutachimba visima vitatu kwa  huko Mtwara  

Pia alisema kwa kila makampuni kumi ambayo yanawekwa kwenye kazi tutahakikisha zaidi ya makampuni sita yatakuwa ya kitanzania ili kuhakikisha watanzania wanafaidika